Alhamisi, 19 Mei 2016

Swaumu

FAIDA ZA FUNGA

MTUME MUHHAMADI  rehema na amani ziwe juu yake amesema :: FUNGENI MPATE AFYA

pindi unapo kula chakula mfumo wa mmengenyo wa chakula huvunja vunja CARBOHYDRATE  kuwa katika GLUCOSE(sukari) kwa ajili ya kuupa nguvu mwili hivyo glucose hufyonzwa kutoka katika njia za mmengenyo na kupelekwa katika damu kisha huenda mpaka kwenye cell na kuzalisha nguvu na kujenga mwili

sasa usipo kula mwili hupungukiwa na glucose katika damu na hapo huanza kutafuta stoo (store) ya mwili inayo itwa GLYCOGEN na gylcogen inapo ishiwa basi huchoma mafuta na misuli iliyo ongezeka ili kuupa mwili nguvu.
  kwa hiyo kutokana na hayo maelezo hapo juu utajua zaid faida ya kufunga kama ifaatavyo

© tibazakissuna.blogspot.com

1) HUTIBU MARADHI YA MOYO

Kama tulivyoona kua mafuta mwilin hutumika kwa wingi pindi unapo kua umefunga hivyo kwa muda wa masiku 29 mpaka 30 utakua na selli zenye mafuta CHACHE na kufanya moyo kufanya kazi ipasavyo

2) HUPUNGUZA UZITO

Kwa watu walio wanene na wenye vitambi hii ina maana kua GLYCOGEN (stoo ya chakula katika  mwili ) ni kubwa hivyo unapo funga glycogen zenu zitatumika ipasavyo na kufanya mwili kupungua

3) HUTIBU KISUKARI TYPE 2

katika ugonjwa huu selli za mwilim hua sio sikivu kwa insulini (kidhibiti cha glucose katika damu)  hivyo mtu akifunga insulini hua na nguvu (sensitive) ya kutuma signal  kuiambia GLUCOSE KISAFIRISHI kusafirisha glucose katika seli  kwani ugonjwa huu hutokea pale SIGNAL hiyo inapo zuiwa na kusababisha selli kuto chukua sukari hiyo hivyo hulepelekea sukar kuwa juu

4) HUTIBU KIHARUSI NA MISTUKO

Unapo funga mfumo wako wa moyo na mishipa (cardiovascular) hufanya kazi vyema na kutibia magonjwa yalio katika mfumo huo sasa kama tunavyojua kama  mfumo wako wa damu utafanya kazi vyema inamaana uwezo wa ubongo kupata oxygen ya kutosha utakuepo hivyo ubongo utafanya kazi ipasavyo

5) HUPUMZISHA MMENGENYO

Maradhi mengi hukulia na kukomaa katika mfumo wa mmengenyo na kisha husambaa kwenye damu pindi mmengenyo unapo kua umepumzika hali ya vijidudu vinavyo leta maradhi hufaa na mwili kujisafisha kupitia metabolism

6) HUONGEZA UMRI

ni kweli kua kula bila kushibisha tumbo hukuongezea umri wa afya njema katika maisha hivyo ubora wa kufunga ni mara mbili yake

7) HUKUZA UWEZO WA UBONGO (akili)

kufunga imethibitishwa kuongeza uwezo wa ubongo kwani husaidia kuzalishwa kwa protein inayoitwa ( brain-derived neurotrophic factor (BDNF.)} kutoka 50 mpaka 400 ambayo husaidia kulinda ubongo kutokana na mabadiliko na pia kuzalisha neurons

© tibazakissuna.blogspot.com

8) HUTIBU NGOZI NA CHUNUSI

kwakua mwili unapata pumziko la kusaga na kusambaza chakula basi huamishia nguvu zake katika kujenga mwili na kuuboresha haswa kuanzia kwenye ngozi

9) HUKUTIBUA ASTHMA NA MATATIZO YA USINGIZI

funga huweza kuonda tatizo hili kwa kupunguza chumvi na maji mwilini na pia hupunguza uvimbe wa tissue hali inayo weza msaidia mtu kulala vyema na kuondosha shida ya kupumua

10) HUTIBU NAFSI

#TABIA huanza kama uamuzi kisha hua Tabia ambapo hukua na kua mraibu/teja (addicted)  na utajua kua upo addicted pindi unapo taka kuliacha jambo hilo na kushindwa hapo jua upo katika hali ya addiction
Allah mjuzi zaidi ila ili kuibadilisha tabia ya mtu huchukua masiku 30

hivyo REHAB ( sehemu za kurekebisha tabia ) hua ni siku 30 na WAISLAM tunafunga siku 29 mpaka 30
hivyo miongoni mwetu tuna ingia kufunga ili kutibu maradhi yaliyo ingia katika nafsi mfano

KUVUTA SIGARA BANGI NA UNYWAJI POMBE

KUJICHUA > njia hii hua ni njia bora zaid ya kujikinga kwani mfumo wa divide and conquer huingia vyema katika swala la funga na kukusaidia kumiliki matamanio yako na kujihifadhi

UZINIFU >  mwenzi huu ni mwenz wa kujihifadhi kwanzia macho mpaka utendaji na ukifunga matamanio hupungua kwa kiasi kikubwa wanasayansi wamethibitisha hili kua njia nyepes na yenye kusaidia bila madhara

KUSENGENYA NA KUTUKANA > mwenzi huu hukupa haya na aibu ya kufikiria mara mbili jambo kabla hujaliendea jambo hivyo hukufunza aibu ukiwa na AIBU UNAKUA NA ADABU

HIVYO KUA MKWELI KWA SWAUMU YAKO ISHIKE NAFSI YAKO NA UTAPONA KWA UWEZO WA ALLAH MARADHI YA NAFSI NDANI YA MASIKU 29 MPAKA 30
© mketo.blogspot.com

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni