Alhamisi, 19 Oktoba 2017

Mfaham mshirikina

السلام عليكم ورحمة الله وبركاته.

*ALAMA ZA KUMJUA MGANGA  (MSHIRIKINA) MCHAWI.*

Amesema Allah mtukufu.

ۖ إِنَّهُ مَن يُشرِك بِاللَّهِ فَقَد حَرَّمَ اللَّهُ عَلَيهِ الجَنَّةَ وَمَأواهُ النّارُ ۖ وَما لِلظّالِمينَ مِن أَنصارٍ.

Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharamishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru (Almaaidah 72).

*Zifuatazo ni alama zinazo julisha mganga mshirikina.*

(a) Ni kuuliza jina la mgonjwa au mama yake au baba yake ili imsaidie kujua maradhi ya mgonjwa na kumtibu.

(b) Kutaka athari kwa mgonjwa kama nguo yake au nywele au kucha na kadhakika.

(c) Kumpa mgonjwa hirizi yenye mchoro na maandishi ya herufi za mkato  au karatasi yenye maandishi hayo na kumtaka atie ndani ya maji kisha anywe.

(d) Kusoma visomo visivyo sikika au lugha inayo tumika haieleweki.

(e) Kumtaka mgonjwa alete mnyama au ndege mwenye sifa maalumu na kumchinja bila ya kumtaja Allah, *(Bismillaahi)*

(f) Kumpa mgonjwa makaratasi ili ayachome moto au achimbie ardhini au atundike juu.

(g) Kumpa sharti mgonjwa asiguse maji kwa muda maalumu.

(h) Kumwambia mgonjwa jina lake na jina la mzazi wake na kumtajia kilicho mleta kwake mtu huyo.

(i) Kuwa matamshi yake ni kutaka msaada kwa Majini kama kuita *Yaa Sybiyaan wamakataan* na kadhalika.

(j) Kumtenga mgonjwa na watu kwa muda maalumu kwa kukaa chumbani tena kwenye kiza chumbaa kisicho pitisha hata mionzi ya jua.

*Ametukataza Mtume swalla llaahu alayhi wasallama kuwaendea waganga wenye sifa za ushirikina*.

أن النبي صلى الله عليه وسلم قال "من أتى كاهنا أو عرافا فصدقه بما يقول فقد كفر بما أنزل على محمد صلى الله عليه وسلم" (رواه أحمد.)

Hakika Mtume swalla llaahu alayhi wasallama amesema, Mwenye kumuendea Kuhani au mpiga Ramli na akamsadikisha ayasemayo, hakika amekufuru kile kilicho teremshiwa kwa  Muhammadi swalla llaahu alayhi wasallama (Ameipokea Ahmadi).

ٌقالَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلمَ:"مَنْ أتى عَرَّافًا فَسَأَلهُ عَنْ شَئٍ لم تقْبَل لَهُ صَلاةُ أربعينَ ليلة(رواه مسلم).

Amesema Mjumbe wa Allah swalla llaahu alayhi wasallama, Mwenye kumuendea mpiga Ramli, kisha akamuuliza jambo, hatokukubaliwa Swala siku arobaini (Ameipkea Muslimu).

*Akili za kuambiwa changanya na zako,*

*Allah atuhifadhi na mitihani ya washirikina.*

*آمين*.

Jumatano, 18 Oktoba 2017

Kubemenda

Kubemenda Mtoto

Kumbemenda mtoto ni mtoto kutokua vizuri ikidhaniwa kutokea kutokana na mama anayenyonyesha mtoto kukutana kimapenzi na mwenzi wake hasa kipindi mtoto bado ni mchanga na ananyonyeshwa. 

Hii ni dhana iliyopo katika jamii mbalimbali, na inadhaniwa hutokea kwa sababu mtoto kunyonya maziwa yenye mbegu za kiume zilizoingia kwenye maziwa baada ya kufanya mapenzi. 

Je, kuna ukweli wowote? 
Hapana. kiukweli na kiutaalamu dhana hii si sahihi kabisa! 
kufanya mapenzi na mwenzi wako baada ya kujifungua hakuwezi kusababisha afya ya mtoto kuzorota. mwanamke anapokutana na mwanaume kimapenzi, shahawa huingia kwenye tumbo la uzazi na kubaki huko. haziingii kwenye damu wala haziwezi kufika kwenye maziwa. dhana ya kuwa shahawa huingia kwenye maziwa na kumuathiri mtoto sio sahihi. 

Ni baada ya muda gani mwanamke aliyejifungua anaweza kufanya mapenzi? 
unaweza kuanza kufanya mapenzi tena baada ya maji maji yenye damu ya uke (lochia) kuacha kutoka ambayo ni kama wiki 3 mpaka 4 baada ya kujifungua, na wewe kujisikia vizuri na kuwa tayari kushiriki katika mapenzi. pia, mnaweza kusubiri mpaka wiki 6 zipite toka ulivyojifungua. 

Je, kuna athari yoyote ya kufanya mapenzi baada ya kujifungua? 
Kufanya mapenzi baada ya kujifungua hakuwezi kuleta madhara kwa mtoto endapo hamna maambukizi ya magonjwa kama virusi vya ukimwi (vvu). ikiwa mwanaume ana vvu anaweza kumuambukiza mama na kisha mtoto kuambukizwa kupitia maziwa ya mama. 

Ikiwa mnafanya mapenzi kabla ya damu damu ya ukeni kukata, maambukizi ya bakteria yanaweza kutokea kwenye tumbo la uzazi (endometritis). pia kuna uwezekano wa mama kupata ujauzito miezi 6 ya kwanza ya kunyonyesha. 

Nini kinasababisha afya ya mtoto kuzorota? 
Kama tulivyoona, kufanya mapenzi hakusababishi mtoto kubemendwa. afya ya mtoto inaweza kuzorota kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo; 

Kukosa maziwa ya mama ya kutosha

Mtoto kushindwa kunyonya vizuri

Kuanzishiwa vyakula vya ziada mapema, kabla mtoto hajafikisha miezi 6 au vyakula visivyo na viritubisho vya kutosha.

Homa, nimonia na maambukizi ya mfumo wa mkojo (uti) za mara kwa mara.

Maambukizi ya magonjwa kama virusi vya ukimwi (vvu) au kifua kikuu.

Matatizo ya moyo ya kuzaliwa nayo (congenital heart diseases).

Kufanya mapenzi na mwenzi wako hakusababishi mtoto kubemendwa. baada ya kujifungua mtoto hutegemea kupata lishe bora kutoka kwenye maziwa ya mama, hivyo nyonyesha mtoto wako vizuri. ukiona ukuaji wake unazorota, onana na daktari.

Jumanne, 10 Oktoba 2017

Mshirikina

السلام عليكم ورحمة الله وبركاته.

*ALAMA ZA KUMJUA MGANGA  (MSHIRIKINA) MCHAWI.*

Amesema Allah mtukufu.

ۖ إِنَّهُ مَن يُشرِك بِاللَّهِ فَقَد حَرَّمَ اللَّهُ عَلَيهِ الجَنَّةَ وَمَأواهُ النّارُ ۖ وَما لِلظّالِمينَ مِن أَنصارٍ.

Kwani anaye mshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharamishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na walio dhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru (Almaaidah 72).

*Zifuatazo ni alama zinazo julisha mganga mshirikina.*

(a) Ni kuuliza jina la mgonjwa au mama yake au baba yake ili imsaidie kujua maradhi ya mgonjwa na kumtibu.

(b) Kutaka athari kwa mgonjwa kama nguo yake au nywele au kucha na kadhakika.

(c) Kumpa mgonjwa hirizi yenye mchoro na maandishi ya herufi za mkato  au karatasi yenye maandishi hayo na kumtaka atie ndani ya maji kisha anywe.

(d) Kusoma visomo visivyo sikika au lugha inayo tumika haieleweki.

(e) Kumtaka mgonjwa alete mnyama au ndege mwenye sifa maalumu na kumchinja bila ya kumtaja Allah, *(Bismillaahi)*

(f) Kumpa mgonjwa makaratasi ili ayachome moto au achimbie ardhini au atundike juu.

(g) Kumpa sharti mgonjwa asiguse maji kwa muda maalumu.

(h) Kumwambia mgonjwa jina lake na jina la mzazi wake na kumtajia kilicho mleta kwake mtu huyo.

(i) Kuwa matamshi yake ni kutaka msaada kwa Majini kama kuita *Yaa Sybiyaan wamakataan* na kadhalika.

(j) Kumtenga mgonjwa na watu kwa muda maalumu kwa kukaa chumbani tena kwenye kiza chumbaa kisicho pitisha hata mionzi ya jua.

*Ametukataza Mtume swalla llaahu alayhi wasallama kuwaendea waganga wenye sifa za ushirikina*.

أن النبي صلى الله عليه وسلم قال "من أتى كاهنا أو عرافا فصدقه بما يقول فقد كفر بما أنزل على محمد صلى الله عليه وسلم" (رواه أحمد.)

Hakika Mtume swalla llaahu alayhi wasallama amesema, Mwenye kumuendea Kuhani au mpiga Ramli na akamsadikisha ayasemayo, hakika amekufuru kile kilicho teremshiwa kwa  Muhammadi swalla llaahu alayhi wasallama (Ameipokea Ahmadi).

ٌقالَّ رسولَ اللهِ صلى الله عليه وسلمَ:"مَنْ أتى عَرَّافًا فَسَأَلهُ عَنْ شَئٍ لم تقْبَل لَهُ صَلاةُ أربعينَ ليلة(رواه مسلم).

Amesema Mjumbe wa Allah swalla llaahu alayhi wasallama, Mwenye kumuendea mpiga Ramli, kisha akamuuliza jambo, hatokukubaliwa Swala siku arobaini (Ameipkea Muslimu).

*Akili za kuambiwa changanya na zako,*

*Allah atuhifadhi na mitihani ya washirikina.*

*آمين*.

Jumatatu, 9 Oktoba 2017

Mafuta ya nazi

Faida 10 za kutumia Mafuta ya Nazi

1. Mafuta ya nazi kwa afya ya Moyo: 
Mafuta ya nazi yana asidi mhimu sana kwa afya ya moyo iitwayo ‘lauric acid’ ambayo ina uwezo mkubwa kuuweka moyo wako katika hali ya afya na furaha kwa kuidhibiti kolesteroli/lehemu mbaya katika moyo na mwili kwa ujumla. Lauric acid huongeza uwepo wa kolesteroli nzuri mwilini ijulikanayo kwa kitaalamu kama High Density Lipoprotein (HDL) huku ikiishusha ile kolesteroli mbaya ijulikanayo pia kwa kitaalamu kama Low Density Lipoprotein (LDL) jambo ambalo ni mhimu kwa afya ya moyo kama anavyosema Lovisa Nilsson, mtaalamu wa lishe wa Lifesum. 

2. Mafuta ya nazi huuongezea nguvu mfumo wa mmeng’enyo wa chakula: 
Hii ndiyo moja ya faida ya mafuta ya nazi niipendayo zaidi. Ndiyo mafuta ya nazi yanayo uwezo kusaidia kudhibiti uzito uliozidi kwa sababu mafuta haya ni mepesi kumeng’enywa na hayagandi kama yalivyo mafuta mengine mazito (fatty acids) jambo linalosaidia kuuondoa uzito uliozidi mwilini. Kutokana na kitendo hiki cha kuongeza uwezo wa mwili kukimeng’enya chakula, watu wanaoyatumia mafuta haya kupikia vyakula vyao kila siku kwa kawaida huwa na uzito wa kawaida. Anasema Geeta Sidhu Robb, mtaalamu wa lishe na mwanzilishi wa Nosh Detox. 

3. Mafuta ya nazi hung’arisha ngozi: 
Siyo sehemu za ndani tu ya mwili zinazofaidika na mafuta haya ya nazi kama yanavyofanya mafuta mengine ya asili, kama unataka kuwa na ngozi nzuri yenye mng’aro na yenye afya na yenye muonekano wa asili basi paka mafuta ya nazi kila siku kwenye ngozi yako, mafuta ya nazi yana uwezo mkubwa katika kuua bakteria, virusi, na vijidudu vya aina yeyote vinavyoweza kuidhuru ngozi, haya ni mafuta kwa mwili mzima yaani pakaa kwenye ngozi yote usoni, mwilini, kwenye nywele na kwenye kucha. Pia unaruhusiwa kuyatumia mafuta haya wakati wa masaji. 

4. Huongeza nguvu mwilini: 
Mafuta ya nazi ni chanzo kizuri cha nguvu ya mwili kwani yana sifa ya kuelea kwa kiasi kidogo kwenye damu ‘medium chain triglycerides – MCT’ ambapo sifa hii huyafanya kusafirishwa moja kwa moja hadi kwenye ini ambako hutumika kama chanzo cha haraka cha nguvu au hubadililishwa kuwa ‘ketones’ ambacho ni chakula cha ubongo. Kwahiyo ikiwa unatafuta lift ya kuinua nguvu yako basi chukua kijiko kimoja cha chai cha mafuta ya nazi weka kwenye kikombe chako cha juisi au uji na utaona maajabu. 

5. Ni mafuta mubadala ya kupikia yenye afya: 
Tofauti na mafuta ya alizeti au hata mafuta ya zeituni, kupika chakula kwa mafuta ya nazi ni zaidi ya afya. Mafuta haya yana uwezo mkubwa wa kuungua na bado yakabaki na viinilishe vyake kama kawaida hata baada ya kuunguzwa au kuchomwa katika moto, hii ni kwamba mafuta kama ya zeituni ambayo huweza kuliwa hata yakiwa mabichi lakini yanapochomwa katika moto basi ubora wake hupungua au kwa maneno mengine huzalisha taka sumu kama ilivyo kwa vitu vingi vinapounguzwa lakini hili halitokei kwa mafuta ya nazi! 

6. Ni mafuta mazuri kwa wasiopenda kutumia mafuta yatokanayo na wanyama: 
Siyo kupika tu na mafuta ya nazi ndiko huleta afya, bali pia ni mafuta mazuri kwa wasiopenda kutumia mafuta yatokanayo na wanyama kama mubadala kwa siagi au vitu vingine mnavyopaka juu ya mikate mnapokula. Hii nikwa sababu mafuta ya nazi hubaki kuwa magumu hata katika joto la kawaida la chumba tofauti na mafuta mengine. 

7. Huzuia maradhi mengi hatari mwilini: 
Kama ilivyo katika kuipunguza kolesteroli, mafuta ya nazi yanao uwezo mkubwa katika kuzuia na kutibu magonjwa mengine sababu ya kuwa na kiasi kingi cha asidi iitwayo lauric acid. Utafiti mwingi umeendelea kuthibitisha kuwa hii lauric asidi hubadilishwa kuwa asidi mafuta nyingine ijulikanayo kwa kitaalamu kama ‘monolaurin’ ambayo inayo sifa ya kudhibit na kuvizuia baadhi ya virusi ikiwemo vile vya ukimwi kuziingia na kuzidhuru seli za mwili na kusababisha maradhi mwilini. Ili kutibu virusi vya ukimwi inashauriwa kunywa glasi 4 za tui la nazi kila siku kwa muda wa miezi mitatu mine na utaona maajabu. 

8. Hutibu tatizo la kupoteza kumbukumbu: 
Hii inaweza ikakushangaza kidogo unapoisikia kwa mara ya kwanza lakini tafiti nyingi zimeonyesha kuwa mafuta ya nazi yanao uwezo kuziamusha seli na shughuli za ubongo na katika kufanya hivyo kutasaidia kuzuia matatizo ya uwendawazimu au ukichaa (dementia) na kupoteza kumbukumbu (Alzheimer). 

9. Hutumika kulainisha uke mkavu: 
Mafuta ya nazi yana matumizi mengi sana mwilini zaidi ya 100, kuna wanawake wana tatizo la kuwa na uke mkavu muda wote hata wakisisimuliwa vipi bado huwa wakavu, kuondokana na tatizo hilo pakaa mafuta ya nazi katika uke wako na utaona faida yake tena bila madhara yeyote hasi. 

10. Husaidia katika ugonjwa wa mzio/aleji: 
Tukisema tuelezee faida zote za mafuta ya nazi kwa hakika hatutaweza, moja ya faida zake zinazoshangaza wengi ni uwezo wa kudhibiti dalili za ugonjwa wa aleji, kila siku pakaa mafuta ya nazi ndani ya pua zako na uone kama utapiga chafya unapokuwa karibu na kile kinachokuletea aleji/mzio. 

MHIMU: Hakikisha unapata mafuta ya nazi ambayo ni ya asili kwa asilimia 100, ikiwa utanunua dukani kuna uwezekano mkubwa yakawa yamechanganywa na kemikali zingine au haidrogeni kitu kinachoyapunguzia thamani ile ya asili. Kama unapikia kwenye chakula najuwa wengi mnapenda wali wa nazi au hata tui lake likiwekwa kwenye samaki au hata mboga yoyote lazima utajing’ata ulimi, basi nakushauri usichanganye na mafuta mengine kwenye hicho chakula.